Marine Le Pen apatikana na hatia ya ubadhirifu wa fedha
31 Machi 2025Matangazo
Le Pen alikuwepo mahakamani wakati hakimu anayesimamia kesi hiyo Benedicte de Perthuis alipoanza kusoma hukumu hiyo, mchakato ambao unapaswa kuchukua chini ya saa mbili.
Hukumu bado haijatolewa
Jaji bado hajatoa hukumu ingawa waendesha mashatka wanataka apewe kifungo cha miaka 5 jela na marufuku ya miaka 5 ya kushikilia afisi ya umma.
Le Pen angojea hukumu ya ubadhirifu wa euro milioni saba
Jaji huyo amesema kuwa itachukuwa muda na kwamba kama desturi, mahakama hiyo itatoa, maelezo kadhaa kuhusu uamuzi uliochukuliwa.
Katika chapisho katika gazeti la La Tribune Dimanche hapo jana, Le Pen alisema kuwa uamuzi wa kesi hiyo, unawapa majaji haki ya maisha ama kusambaratishwa kwa harakati zao.