Marekani yafikia makubaliano na Wahuthi wa Yemen
7 Mei 2025Matangazo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Badr Albusaidi, alisema majadiliano na mawasiliano ya hivi majuzi, na juhudi muhimu zimesababisha kufikiwa kwa makubaliano kusitisha mapigano kati ya pande hizo mbili.
Soma pia: Waasi wa Huothi washambulia kwa kombora Israel
Saa chache kabla ya tangazo hilo, Rais Donald Trump wa Marekani alisema nchi yake itasitisha kuwashambulia waasi wa Houthi baada ya kundi hilo kuridhia kutozighasi tena meli za mizigo.
Kwa karibu wiki saba zilizopita Washington imekuwa inafanya mashambulizi makali ndani ya Yemen ambayo yamesababisha vifo vya watu 300.
Hata hivyo, viongozi wa Wahouthi wamesema pamoja na makubaliano hayo na Marekani, kundi hilo halitositisha mashambulizi yake yanayoilenga moja kwa moja Israel.