MigogoroAfrika
Marekani yawaamuru wafanyakazi wake kuondoka Sudan Kusini
9 Machi 2025Matangazo
Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema makundi yanayohusika katika mapigano ya sasa ni ya kisiasa na kikabila. Imeongeza kuwa tayari silaha zimeshaufikia umma.
Soma zaidi: Hofu ya kufutika kwa makubaliano ya kupatikana amani Juba
Jumamosi, Tume ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ilisema ongezeko la machafuko na msuguano wa kisiasa nchini Sudan Kusini, unatishia mchakato tete wa amani.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa nchini humo Yasmin Sooka, alitoa wito kwa viongozi wa Sudan Kusini kuzingatia tena haraka harakati za kudumisha amani, kuheshimu haki za binadamu na kuhakikisha hakuna vikwazo kuelekea kwenye demokrasia.