JamiiPakistan
Mamlaka za Pakistan zapambana kunusuru wakazi na kimbunga
13 Juni 2023Matangazo
Mwenyekiti wa mamlaka ya taifa ya kusimamia majanga,Luteni jenerali Inam Haider Malik amewaambia waandishi habari katika mji mkuu Islamabad, kwamba zoezi la kuhamisha watu litakamilisha alhamisi asubuhi. Kiasi watu 26,000 wameshahamia kwenye maeneo salama kufikia sasa.
Wakaazi wapatao 100,000 kutoka maeneo ya ukanda wa pwani ya Pakistan wanahitaji kuhamishwa kabla ya kimbunga kibaya hakijapiga katika mkoa wa Sinh,na ambacho hakijawahi kushuhudiwa kwa miaka 25. Kimbunga hicho kinatarajiwa kupiga tarehe 15,Juni.