Mamilioni warejea nyumbani baada ya Tsunami kupungua
31 Julai 2025Matangazo
Baada ya mojawapo ya matetemeko makubwa zaidi ya ardhi kuwahi kurekodiwa kukumba eneo hilo mataifa kuanzia Japan hadi Marekani na Ecuador waliwataka wakazi kuondoka kwenye maeneo ya pwani.
Tsunami ilisababisha usumbufu mkubwa, Peru ikifunga bandari 65 kati ya 121 za Pasifiki na mamlaka za Maui kuahirisha safari za ndege kwenda na kutoka kisiwa cha Hawaii.
Lakini baada ya hofu ya kutokea maafa kupungua, nchi hizo zilianza kuondoa tahadhari au kushusha kiwango cha kitisho na kuwaambia wakazi wa pwani kuwa wanaweza kurejea.