JamiiVatican
Mamia ya waumini wazuru kaburi la Papa Francis
27 Aprili 2025Matangazo
Mamia ya waumini walipanga foleni mapema leo mbele ya kanisa hilo kabla yakufunguliwa saa moja asubuhi kwa majira ya Vatican.
Baraza litakaolomchagua mrithi wa Papa Francis linatarajiwa kuzuru kaburi hilo saa kumi jioni na kufanya sala za jioni katika eneo hilo.
Soma pia: Takriban watu 200,000 wahudhuria mazishi ya Papa Francis
Papa Francis alichagua kuzikwa katika kanisa hilo katikati mwa Roma badala ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro huko Vatican walikozikwa watangulizi wake wengi.
Papa Francis alizikwa jana baada ya hafla kubwa katika uwanja wa Mtakatifu Petro iliyohudhuriwa na maelfu ya waumini pamoja na viongozi wa dunia.