Mamia ya watu wahudhuria misa maalum kumuombea Papa
25 Februari 2025Matangazo
Watu hao walikusanyika katika mji alikozaliwa wa Buenos Aires wakati akiwa askofu mkuu kabla ya kupewa upapa, alipokuwa akiongoza misa na kupinga ukosefu wa usawa na dhulma.
Taarifa ya Vatican imesema hali ya kiafya ya kiongozi huyo wa kidini bado sio ya kuridhisha japo imeimarika kidogo.
Leo ni siku ya 11 kwa Papa Francis mwenye umri wa miaka 88, tangu alipolazwa hospitali, ikiwa ndio muda mrefu zaidi kukaa hospitali katika muda wa karibu miaka 12 aliyohudumu kama Papa.